Sheria

Mfumo wa Haki za Watoto Somalia

By Khadija Mbesa Sheria ya kiislamu, sheria ya kimila, na sheria ya jinai ya kidunia inatumika nchini Somalia, ila hakukuwa na sheria madhubuti, inayofanya kazi ya kitaifa na hakuna marufuku wazi ya adhabu ya kifo, adhabu ya viboko au kifungo cha maisha kwa wakosaji watoto kote nchini.  Sheria ya Mpito ya Shirikisho (TFG) ni serikali inayotambuliwa kimataifa ya Somalia. Mnamo 2009, Bunge la Shirikisho la Mpito, lilipiga kura ili kutekeleza sharia kama sheria ya kitaifa. Kulingana na Rais aliyechaguliwa enzi hizo, hii itakuwa tafsiri ya wastani ya ‘Sharia’. Walakini, TFG inadhibiti sehemu kidogo ya mjii mkuu wa Mogadishu, Maeneo mengine kusini mwa Somalia yapo chini ya vikundi vya upinzani venye silaha, haswa Alshabab na Hizbul Islam, ambazo zinaweka tafsiri kali ya sheria ya kiislamu.   Kaskazini, mkoa unaojitawala wa Puntland na jamhuri ya kujitegemea ya Somaliland ina utulivu zaidi, na serikali zinazofanya kazi na mifumo ya sheria.  Hakuna umri wa chini kabisa, wa uwajibikaji wa jinai nchini Somalia. Kulingana na Kusini au Kati mwa somalia na Puntland, kanuni ya adhabu ya somalia 1962 inaweka umri wa chini wa uwajibikaji wa jinai, miaka 14 na inatoa adhabu iliyotengenezwa kwa watoto wenye umri wa miaka 14 hadi 17. Mahakama ya watoto na sheria ya marekebisho 1970, inafafanua mtoto kama chini ya miaka 14, na kijana kama 14-17. Mahakama hiyo yasema kwamba, korti ya watoto ina mamlaka ya kipekee, ya kusikiliza na kuamua kesi zinazohusiana na watoto pamoja na vijana kuhusu kosa lolote lile, isipokuwa mauaji.   Walakini, inawezekana kwamba, sheria hii haijawahi kutekelezwa na sheria mpya ya watoto inaripotiwa kutungwa huko Puntland. Sehemu ya Somaliland, sheria ya vijana 2007, inaweka umri wa uwajibikaji wa jinai kuwa miaka 15, na inalinganisha vifungu vya sheria ya kidunia, na sheria ya kitamaduni. Walakini, sheria haijatekelezwa kikamilifu na kazi nyingi za korti za chini, katika haki za jinai.  Mambo, haswa yanayohusu watoto, yametekelezwa hivi karibuni na kamati za usalama za mkoa. Wakati wa miaka ya 1980, hukumu zilizotolewa na kamati hizi, ni pamoja na kifungo cha maisha na adhabu ya kifo, japokuwa hivi karibuni, sheria hizo zinaonekana kuwa duni.  (Source 1 )  Hivi sasa, mfumo wa kisheria unaosimamia watoto wanaokinzana na sheria umepitwa na wakati, na hauambatani na mkataba wa haki za Mtoto na vyombo vyovyote vinavyotumika vya kimataifa.  Sheria ya vijana ya 1970 ndio kifungu maalum pekee ndani ya mfumo wa sheria ya Somalia, ambao unasimamia matibabu na usimamizi na kuwekwa kizuizini kwa watoto, ndani ya mfumo wa haki ya jinai.  Kama nilivyosema hapo awali, Somalia haikuwa chama cha Mkataba wa haki za Mtoto (CRC) au itifaki zake za hiari enzi hizo.  Chini ya kifungu cha 59 cha sheria ya adhabu, watoto walio chini ya umri wa miaka 14 hawatakuwa na jukumu la jinai. Umri wa uwajibikaji kwa hivyo huanza baada ya miaka 14.  Hakuna vifungu maalum vinavyoongoza matibabu kwa watoto walioko gerezani, au tawala maalum kwa watoto walioko kizuizini. Walakini, kifungu cha 60 cha sheria hiyo hiyo kinasema kwamba, watoto walio na miaka 14 hadi 18, wanapelekwa gerezani ikiwa wamekamatwa au wamehukumiwa kosa kubwa, ila wakati wa tathmini, mamlaka ya Somalia haikutoa ufafanuzi wowote kuhusu ni kosa gani lililo kubwa.  Kwa hivyo, kuna pengo katika sheria inayotumika kuhusu umri ambao mtoto anaweza kupelekwa gerezani au kuwekwa kizuizini. Mwisho kabisa, watoto waliopatikana na hatia ya makosa madogo, wanaweza kuachwa kwa msamaha ikiwa dhamana itatolewa.  Source; Pg31-33  Ijapokuwa Somalia haikuwa mwanachama wa Mkataba wa Haki za Watoto, mnamo mwaka wa 2015 Somalia ilifanya historia kwa kutekeleza haki za watoto kwa kuwa nchi ya 196  katika kuridhia Mkataba wa Haki za Mtoto (CRC). 

Mila yazika Ndoto za Watoto wa Kike

by Martha Chimilila Ndoa za Utotoni ni ndoa ambazo hufungwa kabla ya wana ndoa kufika umri wa miaka 18. Ijapokuwa sheria zinapinga ndoa za utotoni, lakini tafiti zinaonyesha ongezeko la vitendo vya uvunjwaji wa sheria vikiendelea ulimwenguni kote. Ndoa za utotoni zinasababisha matatizo makubwa kama Unyanyasaji wa kijinsia, Kupoteza haki ya kupata elimu na matatizo ya Kiafya.  Nchini Rwanda, sera mbalimbali na pesa zilitolewa ili kutekeleza miradi dhidi ya mapigano ya ndoa za utotoni. Tatizo kubwa ni kwamba wanaharakati wa haki za watoto wamekumbana nalo ni kuwa, jamii inayowazunguka watoto hawa ndiyo ina neno la mwisho. Hii inakwamisha utekelezaji wa adhabu kali kwa watu wanaovunja sheria.   Ili kuweza kupata suluhu za kupunguza ndoa za utotoni nchini Rwanda, wadau mbalimbali na wanaharakati wa haki za watoto wanapaswa washirikiane. Maafisa wa serikali wanaweza kuona kuwa hawawezi kutoa mawazo yenye Utatuzi wa tatizo hili ila viongozi wa Jadi wanaweza. Viongozi wa Jadi wanaweza kutoa suluhu ambazo zitaenda na mahitaji yao, suluhu hizi zinaweza pia kutumika kurekebisha shida nyingine zinazosababisha uvunjwaji huu wa haki za Kibinadamu.  Katika nchi nyingi za Kiafrika viongozi wa Jadi wana ushawishi mkubwa kwani wana taarifa muhimu za ushiriki wa wanakijiji na imani zao maana ni watu ambao wanaishi nao. Wao husikilizwa na Kuheshimiwa na wana kijiji, viongozi wa jadi huungwa mkono kwa kile ambacho watakiongea. Kwa hivyo ni muhimu kutoa mafunzo na kuomba msaada wao katika kusaidia kuzuia ndoa za utotoni.  Nini kifanyike ili Kutatua tatizo;  Ni muhimu pia kutoa mafunzo shuleni ili kuongeza uelewa wa mabinti. Wasichana wengi nchini Rwanda hufikiri ni Kawaida kwao kuolewa wakiwa na umri mdogo. Wakipatiwa mafunzo na kufahamishwa athari za kuolewa katika umri mdogo, wataweza kupinga na hata kukata rufaa katika vyombo vya kisheria.   Ushirikishwaji wa viongozi wa dini utasaidia kupunguza tatizo la ndoa za utotoni. Viongozi wa dini wana ushawishi mkubwa katika kubadili mitazamo ya waumini wao. Wana uwezo wa kutetea uwezeshwaji na ushiriki wa watoto wa kike katika mijadala ya kijamii, hii itasaidia kubadilisha Mitazamo juu ya maswala ya jinsi na jinsia katika jamii na hii itachangia kuongeza thamani kwa watoto wa kike.  Serikali inapaswa kuanzisha idara vijijini ili kushughulikia ndoa za utotoni. Idara hizi zitasaidia kuanzishwa kwa vilabu vya wasichana ambazo zitasaidia kutoa taarifa na kuongeza uelewa wa athari za ndoa za utotoni. Vilabu hivi vitaweza anzisha miradi mbalimbali ambayo itawasaidia watoto wa kike kupata kipato. Umaskini ni kikwazo kikubwa na ndiyo sababu kuu inayochangia ongezeko la ndoa za utotoni.  Source: https://blogs.worldbank.org/youth-transforming-africa/rwandan-communities-have-last-word-ending-child-marriage 

Uchambuzi wa Mfumo wa Haki za Watoto Nchini Tanzania

By Martha Chimilila Tanzania kama zilivyo nchi zingine duniani, inaendeshwa kwa kufuata misingi ya sheria, sera na katiba. Kuna vyombo mbalimbali ambavyo husimamia katiba na sheria mfano mahakama au vyombo vingine vya ulinzi. Katika kutekeleza mikataba mbalimbali inayoletwa na nchi wahisani, mifumo ya sheria za watoto ilipimwa ili kuona ni jinsi gani inaweza kutumika vyema. …

Uchambuzi wa Mfumo wa Haki za Watoto Nchini Tanzania Read More »