By Khadija Mbesa
Unyonyaji wa kijinsia katika safari na utalii una hatari kwa mtoto! Hakuna nchi ambayo haijaguswa na jambo hili na hakuna mtoto asiye na kinga.
Wakati utalii unapoanza tena baada ya kusimamishwa kwa sababu ya janga la corona, serikali inapaswa kuhakikisha kwamba, watoto hawanyanyaswi zaidi wala hawawi waathirika wa unyonyaji wa ngono.
Mgogoro wa kiuchumi, ambao haujawai kutokea kamwe, unaosababishwa na janga la COVID-19 umezidisha ukosefu wa usawa uliopo, na udhaifu wa watoto walio katika hali duni, na hivyo kuongeza hatari za kuwaweka wazi kwa uuzaji, unyanyasaji wa kijinsia na wafanyikazi katika muktadha wa ukarimu na tasnia ya utalii , iwapo ni mtandaoni au nje ya mitandao.
Kenya ikiwa ni moja wapo ya nchi zilizofunguliwa kwa kuwakubali watalii nchini wakati huu wa corona, Inafungua hatari zaidi ya watoto kuwa waathirika wa unyonyaji. Sio suala la jinsia ya mtoto, bali suala hili linajumuisha watoto wa jinsia zote. Neno “beach boys” kule pwani, linamaanisha watoto wa kiume ambao ‘wanatembea’ na watalii, Unaweza pata mtoto wa miaka kumi na minne ni ‘beach boy‘, huyu ni mtoto anayepaswa kuwa shuleni na sio kutembea na watalii. watalii hawa wanawaonyesha watoto kutumia madawa ya kulevya na kuwanyonya kingono.
Na wakati huu wa corona, ambapo kumekua na migogoro ya kiuchumi, watoto wengi walio katika hali ya umaskini, wanawakimbilia watalii ili kupata pesa rahisi ya kuweza kumudu maisha yao.
Kazi ya ngono, inayohusisha pia watoto, inaonekana kama njia inayokubalika ya kupata riziki katika pwani ya Kenya. Kwa wazazi na jamaa,wanaona mtoto aliye na mtalii mzungu kama rafiki wa kike au rafiki wa kiume ndiyo njia ya haraka zaidi ya kuiondoa familia kwenye umasikini. Wasichana na wavulana wadogo wanahimizwa na familia zao kutafuta watalii ambao watahudumia mahitaji ya familia. Hii inamaanisha kwamba, kwa makusudi, familia zitaweka watoto nje ya shule ili kuwakomboa kutafuta ‘kazi‘ fukweni.
Kila mtu ana jukumu la kuzuia unyonyaji wa watoto katika safari na utalii, Serikali lazima zifanye jitihada zaidi za kushughulikia sababu kuu za udhaifu wa kijamii na kiuchumi wa watoto na familia. Tuwalinde watoto kutokana na wanyonyaji, kwani watoto wa leo ndio endeleo la kesho.
Ꭺt Lionheart Spaniels, we аre offering Cavalier King Charles Ꮪpaniel Ⲣuppіes
that you ϲan’t fіnd anywhегe else. We strongly believe that a happy animal wiⅼl give a family a happy
experiеnce too.
We Ƅreed for Sound Temperament, Personality, Conformation,
& Breed Standard. Our Ꮯavalier King Charles Ѕpanils are indoor
and outdoor dogs. They havе access to a large fenced yard
every day where they arre alloԝed too run and play, and our doors are ALWAYS open ffor them. https://lionheartspaniels.com/